Photo studio

Photo studio Focus empire studio

Naomba tushirikiane leo kutaja vifaa muhimu katika utengenezaji wa Filamu ukiacha Camera ambavyo bila ya hivyo huwezi ku...
11/08/2025

Naomba tushirikiane leo kutaja vifaa muhimu katika utengenezaji wa Filamu ukiacha Camera ambavyo bila ya hivyo huwezi kufanya kitu Bora kwenye utengenezaji wa Filamu.
Naanza na Boom mic

Hellow Mabibi na Mabwana!Tunakodisha Camera aina ya Sony a7r iii na Lense ya FE 1.8/50MM kwa bei ya elf 50 tu wahi sasa ...
19/10/2024

Hellow Mabibi na Mabwana!
Tunakodisha Camera aina ya Sony a7r iii na Lense ya FE 1.8/50MM kwa bei ya elf 50 tu wahi sasa tukuhudumie popote tunafika
Kwa mawasiliano zaidi 0676004670.

Hello habari zenu mabibi na mabwana? Ukijiona wewe ni msanii ambae unaweza kuigiza iwe ni kijana,mzee ama mtoto tafadhal...
18/09/2024

Hello habari zenu mabibi na mabwana? Ukijiona wewe ni msanii ambae unaweza kuigiza iwe ni kijana,mzee ama mtoto tafadhali wasiliana nasi kupitia namba 0676004670 au weka namba yako kwenye Comment ili tukutafute tuna project nyingi zinawahitaji nyinyi wasani,asante.

Matangazo kwenye biashara yoyote ile ni sehemu muhimu sana ya kuifanya biashara yako kukubalika na kupata faida nyingi,h...
24/10/2023

Matangazo kwenye biashara yoyote ile ni sehemu muhimu sana ya kuifanya biashara yako kukubalika na kupata faida nyingi,hususani kwenye swala la Movies industry. Bongo movie moja ya changamoto kubwa wanayopitia ni watu ambao hawapendi kujiongeza na kufanya matangazo kila kona ya jiji,kila kona ya nchi na kila kona ya Dunia hivyo swala la kujulikana kwa movie zetu na kufanya vizuri kwenye mauzo ya kifedha linabaki kuwa swala la bahati nasifu kutokana na hatujajipanga ili tufanye vizuri ila tunafanya kwa kujaribu k**a tutafanya vizuri. Hii picha niliokuwekea hapo chini ni moja ya Promotion ya Game ya Spider man ya Playstation 5 hili tangazo lipo mjini sehemu ambayo wanapita watu hivyo wakiwa wanapita na kukiona kitu k**a hicho lazima itahitaji kutaka kujua nini kilichokuwemo ndani ya hilo tangazo hivyo ni lazima ukanunue nakala yako ili utoe maswali mengi uliyokuwa nayo kutokana na lile tangazo uliloliona.

BONGO MOVIE WAMEISHIWA!!Habari zenu wadau wa Page hii?Leo naomba kujadiliana nanyi kwenye maisha ya Bongo movies.Ivi ni ...
12/01/2023

BONGO MOVIE WAMEISHIWA!!

Habari zenu wadau wa Page hii?

Leo naomba kujadiliana nanyi kwenye maisha ya Bongo movies.
Ivi ni kwanini tumeshindwa kabisa kufanya filamu zetu kuwa vizuri ndani na nje ya Nchi zetu?

(1)Maoni yangu mimi tunashindwa kufanya vitu vizuri kwasababu hatupo Serious na vitu tunavyovifanya hii inatokana na kwasababu hatuna chombo/taasisi maalumu kinachosimamia mambo muhimu yanayotakiwa kuonekana kwenye hizi movie hivyo kila mmoja anajivyatulia tu filamu ili mradi aonekane kwenye Tv bila ya kujua kuwa anauwa soko la filamu nchini kwasababu filamu kumi zinazotoka mtu ameangalia 8 zote utopolo kesho na keahokutwa hawezi kuziangalia zile filamu mbili ambazo hajaziona,hiyo ni kwasababu tayari ameshatokwa na hamu ya bongo movies kupitia filamu 8 mbovu alizoangalia.

(2)Kutokuwa na misingi mizuri ya kazi tunazozifanya. Tunatumia kipaji zaidi kuliko elimu ya Darasani. Unapokuwa na kipaji ni vyema ukaongeza kitu ambacho kitaenda sawa na kipaji chako. Mfano mcheza mpira,wapo wengi wenye vipaji ila mazoezi na kusomeshwa mbindu za uwanjani k**a mambo ya kumkaba mchezaji wa timu pinzani ndio kunakufanya uwe bora zaidi kwenye soka

(3)Bajeti ya filamu. Wengi sana hatufanyi kitu kilichobora kwasababu ya bajeti yetu ni ndogo sana na hata baadhi ya cast huwa tunawachukuwa pasipo na malipo ya aina yoyote yale isipokuwa mein character tu ndio anaelipwa

(4)Story zetu ni mbovu na zenye kufanana fanana fanana na nyepesi sana kiasi cha kwamba mtu anaweza kuotea tukio litakalotokea mbele kiuhakika kabisa. Mfano msichana mzuri anaweza kumgonga muuza machungwa na mtu akaotea kuwa baada ya kumpeleka hospitali atampenda na ukakuta ndio hivyo hivyo 😜

(5)Hatupangilii step zetu za kuonyesha filamu husika. Tumekuwa tukifanya step moja tu ambayo ni kufyatua Cid na kuuza,wakati kuna step 1,2,3............
Mfano: kuonyesha Treilar la movie husika ili kuwaamsha watu kwa vionjo vya filamu yako,kuipeleka kwenye majumba ya Cinema,kuipeleka kwenye ma-Tv makubwa makubwa na mwisho wa siku kuivyatua kwenye CID Ili waone jumla jamala.

K**a una maoni zaidi tupia kwenye Comment hapo ili tuiyamshe Bongo movie yetu iliyolala usingizi mzito.

Karibu sana
My No. 0676004670

Canon 5D Mark iii kwa bei ya 3,000,000/=Camera Safi haina tatizo la aina yoyote ile karibu sana.0676004670
28/09/2022

Canon 5D Mark iii kwa bei ya 3,000,000/=
Camera Safi haina tatizo la aina yoyote ile karibu sana.
0676004670

19/08/2021

Tunapiga picha kwa bei rahisi sana.
Picha za Harusini,picha za kipaimara,picha za kitchenpart n.k
Picha zenye Quality na location za kijanja.
Tuone kupitia
WhatsApp No. 0678646565
call/Messege. 0622752675

19/08/2021

FURSA KWA VIJANA.
Habari zenu vijana? Naitwa Othman nikiwa k**a mmiliki wa page hii.
Napenda kutoa fursa kwa vijana wenzangu kwa kuanzisha kundi la sanaa tutakaloliita NEW EPISODE
Hivyo Wavulana kwa Wasichana mnakaribishwa,tuitengenze sanaa yetu kivyengine kabisa kwenye Tasnia ya bongo Movie,k**a jina la kikundi chetu linavyojieleza.

WhatsApp No. 0678646565
Call/Messege. 0622752675

Asanteni

26/02/2020

Hellow waungwana!!
Leo nina jambo napaswa kuongea nanyi kuhusu Video ya Diamond Platnum na Ten. Bila ya shaka nilichokitaja hakiwezi kuwa kigeni kwenu kwasababu asilimia kubwa ya Watanzania humjua Diamond vyema na kufatilia kila anachokitoa kwenye Maisha yake ya Muziki.
Video hii yenye Colabo na Ten makanake ni nzuri sana,video yenye Quality nzuri na kuwa na mambo mengi mzuri yenye kuifanya ukaweza kuirudia kwa kuitazama hata mara ishirini naa video hii.
Tatizo kubwa la video hii ambalo huitaji kumurika kwa tochi ni kuhusu kucheza na fremu najua wengi nimewaacha ila tuendelee mtanielewa,tunapozungumzia fremu ni lile swala la kioo chako cha Tv kuwa na picha yake haijai kwenye kioo kizima bali inafinywa na utando wa rangi nyeusi hivyo picha inakuwa inaonekana katikati baina ya huo utando mweusi wenye kuonekana juu na chini.
Hivyo video hii ya Diamond na Ten makanake tatizo hili limeonekana mara kwa mara likiwa linabadilishana na full frame yaani picha ya nyimbo hii mara inakuwa low frame(kuwa kwenye mabano ya utando mweusi) na full frame(kuwa ipo full bila ya mabano ya utando mweusi)
Nazani hili ni jambo linalotokea mara kwa mara kwenye video zetu za kibongo tuwe makini kwa kweli kwani unapotumia fremu za aina mbili kwenye nyimbo moja inaonesha udhaifu kwa jopo lililokaa kwa ajili ya nyimbo hiyo kwenye mambo ya editing kwani kuna chansi ya mwisho ya kuiyangalia Video kabla haijapelekwa kwenye Tv.
Nashauri tuwe makini watu wanaohusika na utayarishaji wa video k**a Camera man na video editing
Writting by K**an

Address

Kikwajuni
Zanzibar

Telephone

0676004670

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Photo studio posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share