27/03/2026
Mamlaka ya MajiSafi na Usafi wa Mazingira Tukuyu mapema leo tarehe 27/03/2026 wametoa elimu ya huduma ya maji kwa Mabalozi wa mitaa ya eneo la Makandana kuhusiana na huduma ya Maunganisho ya maji, matumizi ya Dira za maji na namna ya utatuzi wa malalamiko ya Wateja.
Aidha, Mamlaka imeomba ushirikiano wa utatuzi wa changamoto ya mivujo kwa kuomba kupewa taarifa kwa kuwa pia imelalamikiwa na Viongozi hao na kuonekana upotevu mkubwa wa maji unatokana na mivujo. Mamlaka imeeleza kuwa imeunda timu itakayokuwa inashirikiana na viongozi hao katika kupita mtaa kwa mtaa kubaini na kuziba mivujo.
Maoni, ushauri na mapendekezo kutoka kwa wajumbe wa kikao yamechukuliwa na Maafisa wa Mamlaka ya Maji kwa ajili ya kuboresha huduma ya maji Tukuyu Mjini hususan Makandana.