31/05/2026
RC Tanga aunda kamati itoe majibu ndani ya siku 5
Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Balozi, Dk. Batilda Buriani, ameunda Kamati maalumu kubaini tukio la kubomolewa makazi ya wananchi eneo la Msakangoto (maisha plus), kata ya Kigombe, jijini Tanga na kusababisha madhara hasa kwa wazee na watoto.
Pia, Dk. Buriani ametoa siku tano kwa kamati hiyo kutoa majibu kuhusu kibali cha kubomoa nyumba za wananchi kimetoka kwa nani, kwakuwa hakuna taarifa zozote za kiongozi wa serikali, mbali ya kuwa amri imetoka mahakamani.
Amesema, mnamo Mei 22. mwaka huu, Dalali wa Mahakama, bila kushirikisha uongozi wowote, alichukua jukumu na kwenda kubomoa makazi hayo, jambo siyo la kiungwana na limeleta mtafaruku kwa wananchi.
Imeandikwa na Hamida Kamchallah, Tanga