26/05/2022
Maisha siyo magumu kiviiile sema sisi ndiyo tunajichanganya tu ๐
Denis Mpagaze
________________________________________
Leo kila mtu anasema maisha ni magumu. Ukimuuliza ni magumu kivipi, atakwambia anadaiwa ada ya mtoto. Alipeleka watoto kwenye shule za gharama kuliko kipato chake halafu anasingizia maisha magumu.
Kwani angempeleka mtoto wake elimu bure angekufa? Usidhani wenzako wanapenda elimu bure. Uwezo ndiyo unapenda twende huko. Ukiishi kulingana na urefu wa kamba yako maisha hayasumbui sana.
Mwingine ametumia kahela kake kote kununua simu ya bei mbaya ili tu wamuone. Sasa sijui wakimuona anapata nini! Haya wamekuona. Kwahiyo? Ona unakosa hata bando la buku jero kwenye simu ya laki sita.
Mwingine kachukua mkopo kanunua gari na wakati uwezo wa mafuta na service hana, siku amekosa mafuta anaanza kulalamika maisha ni magumu. Ona sasa gari lako wanalitumia wenye mafuta. Wakiligonga unadhani watalitengeneza?
Mwingine kapanga nyumba nzuri kwa gharama ya juu zaidi ya kipato chake, mwenye nyumba akija kudai anasema maisha ni magumu, amvumilie. Kwani ukipanga kule kwenye sogea tukae hadi utakapopata pesa za kutosha kuishi kwenye nyumba nzuri utakufa?
Maisha siyo magumu sisi ndiyo wagumu. Tunajitwisha mizigo kuliko uwezo wetu. Umesomea kuendesha magari madogo unataka ukasukume malori. Utaumia.
Mwingine amezima simu siku nzima, michepuko yake inamsumbua, inataka kodi ya nyumba na hela ya kusuka. Huyu naye ukimuuliza atanasema maisha ni magumu.
Unashindwa kuhudumia visivyo vya lazima halafu unasema maisha ni magumu. We vipi??? Kwani usipokuwa na mchepuko utakufa?
Umechukua vikoba kununua vitu usivyovihitaji ili kuwarusha roho wasiokupenda. Haya umewarusha sawa. Kwahiyo? Halafu unanalamika mumeo hakufikishi!
Unajua shida nyingine zinatupata kwa sababu ya ujinga tu.
Fanya majaribio ya kuishi kulingana na urefu wa kamba yako hata kwa mwezi mmoja uone k**a hujafurahia maisha. Haya maisha ni rahisi sana.
Wacha niendelee kujiuzia vitabu yahe, maisha ya maonyesho na maigizo siyawezi mie. Rusha 5,000 nikurushie kitabu cha Ukombozi wa Fikra uongeze kasi ya kufikiri. Mpesa 0753665484.
Wako
Mwl. Denis Mpagaze
Muhenga wa Karne ya 21