27/03/2026
Hapa ni Bonde la Isimila Iringa sehemu bora kabisa ya utalii, Eneo ambalo moja ya kipande kinachovutia zaidi katika Filamu ya Mufasa the Lion King kutoka kwa waataarishaji wa katuni Walt Disney World walikuja kurekodi wenyewe pasipo kutengeneza mandhari pale Holly Wood k**a tulivyo zoea, ambapo mandhari hiyo ilitoa historia kubwa ya Tanzania na kuonesha uzuri wa nchi yetu duniani kote, maamuzi ya Disney ya kurekodi eneo hili la Isimila ilikuwa ni baada ya wao kutazama Filamu ya Royal Tour iliyoongozwa na Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
Kwa Kifupi Mufasa The Lion King ni Filamu ya Katuni inayohusu Maisha ya Wanyama wa Afrika iliyotayarishwa na Disney the world animation ni moja ya filamu iliyovunja rekodi za mauzo tangu ilipozinduliwa rasmi Desemba 2024 huko Marekani na kuoneshwa kwenye majumba ya Sinema na majukwaa ya kidijitali duniani kote, amapo Tanzania imeonekana sana hapo na kufanya watu watamani kuja ona eneo hilo.
Nimetoka Kilometa 500 na kidogo nikitumia zaidi ya masaa saba mpaka kufika eneo hili na kupiga kambi na Kamera zangu kwa lengo moja tu kukusogezea uzuri wa Bonde la Isimila ili nawe Mtanzania mwenzangu upate Shauku ya kuja kujionea mambo mengi usiyo yafahamu, nitakupitisha kila kona ya eneo hili fuatilia hapa.
Eneo hili kwa sasa linasimamiwa na Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA)