Norman johnz

Norman johnz Entertainment art

Tanzanite bridge 🇹🇿 on progress ✌️
13/12/2021

Tanzanite bridge 🇹🇿 on progress ✌️

08/04/2019

SHE IS MY BEST FRIEND
Simulizi nyingine nzuri itakujia hivi punde kwenye timeline yako, mtunzi: ASELI GB (Norman Johnz)

07/04/2019

Nini ulichojifunza katika simulizi ya THE FLIGHT TO LOS ANGELES
Toa funzo lako........

06/04/2019

Sehemu ya mwisho (the flight to Los Angeles)
Created by ASELI GB (Norman Johnz)
Endelea nayo
Basi baada ya Victoria kuisoma barua ile Trevor alimpelekea mama yake lakini mama yake alijua Kila kitu sababu kabla ya Traves kuondoka alimuaga mama yake, "he left a gift"(aliacha zawadi) Gabriella alimwambia Trevor, "a gift for whom"(zawadi ya Nani) Trevor aliuliza Kisha Gabriella akamwambia "for you and your wife"(ya kwako na mke wako) baada ya hapo Gabriella alikwenda kuwaonesha zawadi ambayo Traves almewaachia na zawadi hiyo ilikuwa Ni gari aina ya AUDI ,Basi Trevor alifurahi sababu aliamini pacha wake hajaondoka na kinyongo chochote moyoni pia Victoria naye alifarijika sababu aliamini Traves amemsamehe kwa maamuzi aliyochukua,mida ya saa tatu Victoria na mama yake walipanda ndege na kuelekea ufilipino,saa tano na nusu walitua katika kiwanja Cha ndege Cha Manila, ufilipino,walivyoshuka walipanda ndege nyingine ndogo ya kwenda Davao,huko ndiko alikozikwa mzee Fernando trillo ambaye Ni baba mzazi wa Victoria baada ya saa moja walifika Davao halafu wakaanza kueley makaburini, walivyofika kwenye kaburi la mzee Fernando trillo Victoria alihuzunika sana sababu alimpenda sana baba yake lakini bahati mbaya alifariki wakati akiwa na umri mdogo baada ya muda kidogo mama yake Victoria alimuonesha picha ya baba yake , Victoria alianza kulia mama yake alimbembeleza huku naye machozi yakimlenga,Basi waliondoka makaburini Kisha wakaanza kurudi Manila, mida ya saa moja usiku walifika jijini Manila wakalala usiku mmoja kesho yake wakarudi Los Angeles, walivyofika tu Trevor na Victoria walifunga safari kwenda jijini Miami kwa ajili ya kuianza honey moon yao,walivinjari Kule Miami kwa muda wa siku Saba baada ya hapo walirudi Los Angeles kwa ajili ya kuwaaga wazazi wao, Trevor alinunua nyumba iliyokuwa katika jiji la Atlanta kusini mashariki mwa marekani,baada ya kuwaaga wazazi Trevor na Victoria waliondoka kwa furaha kwenda kuyaanza maisha mapya Kule Atlanta,Basi walifika Atlanta na wakayaanza maisha mapya kwa furaha na amani
THE END
Toa maoni yako juu ya simulizi hii ya kusisimua,Nani aliyekuwa na Haki ya kufunga ndoa na Victoria kati ya Traves na Trevor,je Traves alionewa ? Toa maoni yako
Shukrani kwa Mungu aliyeniwezesha kutunga kazi hii,pia nawashukuru wote waliochukua muda wao kusoma simulizi hii na kulike page hii Mungu awabariki wote.
Created by ASELI GB (Norman Johnz)
@2017

06/04/2019

Sehemu ya 36(The flight to Los Angeles) created by ASELI GB (Norman Johnz)
Endelea nayo
Basi Victoria alimnyanyua Traves halafu akamfuta machozi kwa mikono yake Kisha akasema "I'm sorry Traves"(samahani Traves) akawa anaondoka zake, Traves alilia K**a mtoto mdogo sababu hakuamini kilichotokea,alidiriki hata kuvunja mahusiano yake na Shirley kwa ajili ya Victoria matokeo yake Victoria naye amemuacha,Traves aliumia sana aliona K**a maisha yake yameharibika tayari.Siku zilisonga mbele, baada ya wiki tatu ndoa ya Trevor na Victoria ilianza kutayarisha, Trevor alikuwa amekwisha pona majeraha yake yote, Victoria alialika ndugu na jamaa kutoka Hawaii wahudhurie harusi hiyo pia mama yake naye alialika ndugu wa Kule ufilipino wahudhurie harusi hiyo, Trevor na Victoria walifurahi sana sababu ilikuwa Ni siku maalumu kwao lakini kwa traves ilikuwa Ni siku ngumu kwake sababu mwanamke ampendaye anafunga ndoa na pacha wake,siku ya harusi ilipofika Traves hakutaka hata kuhudhuria harusi hiyo,Basi harusi ilifanyikia palepale nyumbani kwa Gabriella sababu nyumba ilikuwa na eneo kubwa, hivyo ilikidhi mahitaji ya sherehe hiyo, baada ya Trevor na Victoria kuvishana Pete walielekea ufukweni, walifurahi huku wakipiga picha za ukumbusho wa ndoa hiyo baada ya hapo walirejea nyumbani mida ya saa mbili usiku.kesho yake mama yake Victoria alipanga ampeleke mwanaye ufilipino ili akamuoneshe kaburi la baba yake mzazi lakini kabla ya kuondoka ujumbe alioucha Traves ulikutwa ndani ya nyumba, Traves aliandika ujumbe ufuatao
"Congratulations bro, congratulations Victoria, I'm really happy and proud of your wedding cause it's a special event for you and even for me.the thing that I want to say is that I wish you a joyful life,may be you'll never see me again cause I've traveled to Sydney, Australia
I love you bro,I love you Victoria good luck, your brother and brother in law TRAVES MANUEL WI******ER.
(Hongera Kaka,hongera Victoria,ninafuraha na ninajivunia ndoa yenu sababu Ni tukio maalum kwenu na hata kwangu, Jambo ninalotaka kusema Ni kwamba nawatakia maisha yenye furaha tell,pengine hamtaweza kuniona Tena sababu nimesafiri kuja Sydney, australia.nakupenda Kaka, nakupenda Victoria,Ni Mimi Kaka na shemeji TRAVES MANUEL WI******ER
Trevor alivyoisoma barua hiyo alienda kumpatia mke wake ambaye Ni Victoria baada ya Victoria kuisoma Trevor alimpelekea mama yake,lakini mama yake alitambua Kila kitu sababu kabla ya Traves kuondoka alimuaga mama yake itaendelea....

05/04/2019

Sehemu ya 35(the flight to Los Angeles)
Created by ASELI GB (Norman Johnz)
Endelea nayo
Basi ilipofika jioni Gabriella alikwenda kuzungumza na soledad kuhusu swala la ndoa ya Trevor na Victoria ndipo soledad akamueleza kuhusu Victoria na traves waliyokuwa watoto, alimwambia kuwa traves na Victoria walipendana sana kipindi Cha utoto wao na walitaka wapendane mpaka ukubwani lakini ajali ile ndiyo iliyowatenganisha,hivyo soledad aliomba azungumze kwanza na mwanaye K**a ameridhia kabisa kufunga ndoa na Trevor,Basi alimfuata Victoria Kisha akaanza kuzungumza naye, alimuuliza K**a amekubali kabisa kufunga ndoa na Trevor, Victoria alisema amekubali kabisa,mama yake alijaribu kumuhusisha traves lakini Victoria alisema traves alikuwa Ni rafiki yake wa utotoni istoshe Trevor ameokoa maisha yake wakati Victoria alimueleza mama yake hayo,mama yake aliiona tattoo ya jina la Trevor kwenye mkono wa Victoria ndipo alipotambua kuwa mahusiano ya Trevor na Victoria hayawezi kuvunjika kirahisi sababu yeye alitaka mwanaye afungue ndoa na traves ambaye Ni rafiki yake wa utotoni na sio Trevor, wakati mazungumzo hayo yakiendelea traves alikuwa kando akisikiliza,aliposikia kuwa Victoria anataka kufunga ndoa na Trevor alivunjika moyo kabisa.Baada ya Victoria kumaliza kuzungumza na mama yake alielekea bustanini,alivyofika bustanini alianza kuyachezea maua ghafla Traves alifika eneo lile," why are you doing this to me Victoria"(kwa Nini unanifanyia hivi Victoria) Traves aliongea huku chozi likimtoka, Victoria aligeuka Kisha akasema "I have to do this"(ninatakiwa nifanye hivi) "but...but..but why?(lakini..lakini...lakini kwa Nini) Traves aliongea kwa kujikanyagakanyaga," he saved my life"(ameokoa maisha yangu) Victoria alimwambia huku machozi yakimtoka Kisha akasema "I know that you love me Traves but I have no choice"(najua unanipenda Traves lakini Sina chaguo),Traves alipiga magoti huku akisema "no,no Victoria don't do this to me,I love you more than anything in the world, remember when we were kids you use to tell me that you love me and you'll never leave me"(hapana Victoria usinifanyie hivyo,nakupenda kuliko kitu chochote katika dunia,kumbuka tulipokuwa watoto ulikuwa ukiniambia kwamba unanipenda na hutokuja niacha) Traves aliongea kwa uchungu, mpaka Victoria alianza kulia sana huku akikumbuka wakati wakiwa watoto, ghafla Traves aliiona tattoo kwenye mkono wa Victoria, alivunjika moyo Zaidi, Victoria alimnyanyua Traves halafu akamfuta machozi kwa mikono yake Kisha akasema....

05/04/2019

Sehemu ya 34(the flight to Los Angeles)
Created by ASELI GB (Norman Johnz)
Endelea nayo
"She's my daughter"(Ni mwanangu) soledad aliongea, "are you crazy soledad, your daughter died in the air crash 18 years ago (unawazimu,mwanao alifariki katika ajali ya ndege miaka 18 iliyopita) Gabriella alimwambia soledad,ndipo Victoria alijikuta akianza kulia baada ya kuelezwa yule mama anamaanisha Nini,alilia sana huku akimuuliza kuwa baba yake Yuko wapi, alimwambia alimkuta katika hospitali ya honululu baada ya ajali pia alimueleza kuwa mwili wake yeye haukupatikana,mama yule aliongea kwa uchungu sana sababu alikuwa amekwisha kata shauri juu ya mtoto wake,moyoni mwake aliamini time kwamba mtoto wake yupo hai sababu mwili wake haukupatikana,hata Kule ufilipino walifukia mchanga K**a ishara kuwa Victoria hakupatikana,Basi baada ya muda kidogo Gabriella alianza kumuomba Victoria msamaha baada ya kugundua kuwa Ni mtoto wa rafiki yake,bila kipingamizi Victoria alimsamehe Gabriella Kisha wakakumbatiana baada ya hapo Mamaa soledad Alonso alimuomba Victoria ampeleke kwenye kaburi la mzee Armando aliyemsaidia Victoria baada ya no ajali kutokea.trevor alitakiwa akae hospitalini kwa muda wa wiki mbili baada ya kufanyiwa upasuaji, Victoria, Isabella pamoja na soledad Alonso walikwenda Hawaii kwa ajili ya kulizulu kaburi la mzee Armando baada ya kulizulu kaburi Hilo walirejea Tena Los Angeles.victoria alikuwa Ni mtu mwenye furaha baada ya kuwa pamoja na mama yake sababu alikosa upendo wake kwa muda wa miaka 18 hata soledad Alonso alikuwa na furaha pia baada ya kumpata mwanaye wa pekee.Siku zilisonga sana na hatimaye muda wa Trevor kukaa hospitali uliisha Basi Gabriella alikwenda hospitali kumchukua Trevor, baada ya kufika nyumbani Trevor alimueleza mama yake kuhusu swala la ndoa yake na Victoria, Gabriella alikubali na lilibaki swala la kunieleza mama yake Victoria ambaye Ni soledad Alonso,Basi iliofika jioni Gabriella alikwenda kuzungumza na soledad Alonso

05/04/2019

Sehemu ya 33(the flight to Los Angeles)
Created by ASELI GB (Norman Johnz)
Endelea nayo
Victoria alivyoondoka kidogo mwanamama soledad Alonso alianza kuzungumza na Isabella, alimuuliza "is she your sister?"(je Ni dada yako?) "Yes she's my sister"(ndiyo Ni dada yangu) Isabella alijibu, "your real sister?"(dada yako halisi) soledad Alonso aliuliza Tena, Isabella alimuangalia kwa mshangao Kisha akamuuliza "why are you asking me all these questions?"(kwa Nini unaniuliza maswali yote hayo?) Mwanamama soledad Alonso alishikwa na aibu Kisha akasema alitaka kujua tu, "she's not my real sister"( si dada yangu kabisa) Isabella alimwambia soledad Alonso Kisha akaendelea kusema kuwa yeye hakumbuki vizuri kuhusu Victoria lakini anakumbuka wakati ana miaka sita baba yake alimleta Victoria akiwa amepoteza fahamu alipojaribu kuzungumza na baba yake alimwambia kwamba amemkuta eneo ambalo ndege ilianguka, "where is your home"(nyumbani wapi?) Soledad Alonso alimuuliza Isabella "Hawaii" Isabella alijibu ghafla Victoria akafika "it's time to go Isabella"(Ni muda wa kuondoka Isabella) Victoria alimwambia Isabella ghafla Mamaa soledad Alonso alianza kulia baada ya kutambua kuwa Victoria Ni mwanaye,alilia sana huku akisema "ooooh! Victoria my daughter"(ooooh! Victoria mwanangu), "where have you been"(ulikuwa wapi), Victoria alianza kushangaa pia hata Isabella alianza kushangaa,mama yule alimkumbatia Victoria huku akimsimulia kiss Cha ajali ya ndege iliyotokea miaka 18 iliyopita ambapo alimpoteza mume wake mzee Fernando trillo, ghafla Gabriella,traves na ndugu wengine walifika,walishangaa baada ya kumuona soledad Alonso akilia huku akimtaja Victoria, "what's the problem soledad"(Nini tatizo soledad?) Gabriella alimuuliza rafiki yake ambaye Ni soledad Alonso "she's my daughter"(Ni mwanangu) soledad aliongea, Victoria hakuelewa anamaanisha Nini, " are you crazy soledad, your daughter died in the air crash 18 years ago "(unawazimu soledad,mwanao alifariki katika ajali ya ndege miaka 18 iliyopi

04/04/2019

Sehemu ya 32(the flight to Los Angeles)
Created by ASELI GB (Norman Johnz)
Endelea nayo
Mida ya saa tano asubuhi madaktari waliruhusu mgonjwa kuonana na ndugu zake, Gabriella ndiye aliyekuwa wa kwanza kuingia Kisha akafuata traves ambaye Ni pacha wake Trevor Basi walizungumza naye kwa muda wa dakika kumi na Tano lakini Trevor aliomba azungumze na Victoria, Gabriella alikuwa na kipingamizi lakini hakuwa na jinsi Basi Victoria aliitwa akaingia pamoja na Isabella, Trevor alitabasamu pale tu alipomuona Victoria aliomba apishwe kidogo ili aweze kuzungumza na Victoria,ndugu walinong'onanong'ona huku wakitoka nje,Basi Victoria aliketi karibu na Trevor Kisha akamshika mkono, Victoria alitokwa na machozi ya furaha halafu akasema "thank you Trevor"(ahsante Trevor) "for saving my life"(kwa kuokoa maisha yangu) ,"you don't need to thank me for saving your life"(huitaji kunishukuru Mimi kwa kuokoa maisha yako) Trevor alimwambia Kisha akaanza kumsimulia kuwa wakati hajapata fahamu Kuna ndoto nzuri sana aliota, Victoria alimuuliza ndoto gani?,ndipo Trevor akasema ameota anafunga ndoa na yeye, Victoria alitabasamu tu baada ya hapo Trevor akasema "will you make my dream to become true?"(je utafanya ndoto yangu iwe kweli?) Victoria alibadilika ghafla akaanza kufikiria matukio mbalimbali alikumbuka hata kuhusu traves aliyeharibu ndoa yake kwa ajili yake lakini alipo itazama tattoo kwenye mkono wake Kisha akakumbuka jinsi Trevor alivyopata shida kwa sababu yake,alimuangalia Trevor huku chozi likimtoka Kisha akasema "yes I will"(ndiyo nitafanya) Trevor alitabasamu halafu akasema "thank you Victoria"(ahsante Victoria) ghafla daktari akaingia Kisha akasema mgonjwa anahitaji kupumzika,Basi Victoria alimbusu Trevor shavuni Kisha akatoka nje,alivyotaka nje akakuta ndugu na jamaa wamekwisha ondoka waliobakia walikuwa Isabella na Mamaa soledad Alonso, Victoria aliketi katikati yao, alimsalimu mama yule Kisha akaendelea kuzungumza na Isabella,alizungumza naye kwa muda halafu akaondoka kidogo,alivyoondoka tu, mwanamama soledad Alonso alianza kuzungumza na Isabella, alimuuliza "is she your sister?"(je Ni dada yako?) "Yes she's my sister"(ndiyo Ni dada yangu) Isabella alijibu,"your real sister"(dada yako halisi) soledad Alonso aliuliza Tena Isabella alimuangalia kwa mshangao Kisha akamuuliza "why are you asking me all those questions'(kwa Nini unaniuliza maswali yote hayo) soledad Alonso alishikwa na aibu akasema anataka kujua tu, "she's not my real sister"(si dada yangu halisi) Isabella

04/04/2019

Sehemu ya 31(the flight to Los Angeles)
Created by ASELI GB (Norman Johnz)
Endelea nayo
Basi Victoria alivyofika eneo ambalo ajali ya ndege ilitokea miaka 18 iliyopita,eneo Hilo lilikuwa karibu kabisa na bahari, Victoria alipiga magoti Kisha akaanza kufanya maombi kwa Mungu ili Trevor apate kupona na aendelee kuishi sababu uwezekano wa Trevor kuishi ulikuwa Ni mdogo sana.Huku hospitalini alikolazwa Trevor madaktari walikusanyika katika chumba Cha kufanya upasuaji kwa ajili ya kufanya upasuaji wa mwisho(the final surgery) ambapo Trevor asipozinduka Basi watamuacha afariki moja Kwa moja sababu tatizo lake Ni zito mno,walisubiri kidogo mpaka ilipofika saa mbili na nusu ndipo upasuaji ukaanza kufanyika, Trevor alikuwa na majeraha makubwa sana haswa kwenye mfumo was mkojo ambapo kisu kilipenya Zaidi na kujeruhi sehemu ya kitovu,walirekebisha pamoja na kushona majeraha makubwa.walivyo maliza wakasubiri Kwa muda wa dakika 30 ili mgonjwa azinduke lakini mgonjwa hakuonesha hata dalili ya kuzinduka, madaktari wengi walikata tamaa sababu walitumia ujuzi wao wote kumtibu Trevor lakini Hali imekuwa mbaya Zaidi lakini alikuwepo daktari mmoja ambaye ndiye aliyekuwa mkuu wa team hiyo ya upasuaji hakukata tamaa bado alikuwa na tumaini kwamba Trevor anaweza kuamka, alianza kushtua pumzi ya Trevor maeneo ya kifuani, alifanya hivyo Mara sita lakini Trevor hakuonesha dalili ya kuamka,alivyofanya Mara ya Saba ghafla Trevor alivuta pumzi nzito ndipo akazinduka kwa Kasi huku akipumua haraka haraka, "it's a miracle!"(Ni muujiza) madaktari waliongea kwa mshangao.victoria aliendelea kusali akiwa msituni ghafla wakati akisali alianza kusikia mawimbi ya bahari yana igonga ardhi kwa nguvu ikiashiria kuchafuka kwa bahari Kisha aliiona taswira ya Trevor kwa mbali ikimuita ghafla taswira hiyo ikapotea,Basi Victoria alianza kurudi nyumbani,huku hospitalini madaktari walifurahi sana sababu hawakutegemea Trevor aamke Tena Basi waliwasiliana na familia ya Trevor kwa ajili ya kuwajulisha habari njema juu ya mgonjwa wao.asubuhi ilipofika asubuhi ndugu na jamaa wa Trevor walifika hospitali wakiwa na furaha, Victoria na Isabellawalifi hospitalini wakiwa hawajui lolote kuhusu Hali ya Trevor, walifika hospitalini wakawauliza madaktari kuhusu Hali ya Trevor wakasema anaendelea vizuri kabisa, Victoria na Isabella walikumbatiana huku wakimshukuru Mungu.mida ya saa tano madaktari waliruhusu mgonjwa kuonana na ndugu zake, Gabriella ndiye aliyekuwa wa kwanza kuingia Kisha akafuata traves ambaye Ni pacha

04/04/2019

Sehemu ya 30(the flight to Los Angeles)
Created by ASELI GB (Norman Johnz)
Endelea nayo
Basi Gabriella baada ya kuelezwa kuwa Victoria na Isabella ndiyo waliomleta Trevor hospitali alijua dhahiri kuwa wale vijana aliowaagiza wammalize Victoria wamekwisha haribu kazi,wamemdhuru mwanaye, Gabriella aliogopa sana alihisi Jambo Hilo likija kufichuka atakuwa katika wakati mgumu.Ilipofika mida ya mchana madaktari walitoka nje kwa ajili ya kuwafahamisha ndugu na jamaa wa Trevor juu ya Hali ya mgonjwa,walisema Hali ya mgonjwa Ni mbaya sana na pia wamejaribu kadri ya uwezo wao lakini wameshindwa,ila Kuna daktari alitoa wazo kuwa usiku watafanya nafasi yao ya mwisho na K**a hata pata fahamu Basi watasubiri afe moja kwa moja sababu hakuna njia mbadala, mgonjwa amepoteza damu nyingine sana,wote walishtuka Kisha wengine walianza kulia, Gabriella alianza kujilaumu moyoni huku akijutia kufanya vile,yeye ndiye aliyetuma vijana wawili wakatoe uhai wa Victoria lakini vijana hao walifanya makosa katika kazi, walishindwa kumuua Victoria na badala yake walimdhuru Trevor ambaye aliokoa maisha ya Victoria hivyo endapo Trevor akifariki Basi muuaji Ni Gabriella mwenye ambaye Ni mama mzazi wa Trevor, Gabriella alichanganyikiwa sana hakujua afanye Nini kwa wakati huo.Basi traves na mama yake pamoja na ndugu wengine walienda kulala hotelini huku wakimuombea Trevor apone, Victoria na Isabella walirudi nyumbani wakiwa na majonzi moyoni.matibabu yalitakiwa yaanze mida ya saa mbili na nusu usiku,mida ya saa kumi na mbili jioni Victoria na Isabella walipika chakula Chao Cha jioni Kisha wakala, ilipofika saa moja na nusu Isabella alikwenda kulala lakini Victoria alikuwa na mawazo sana,alikumbuka wakati akifurahi na Trevor kabla ya tukio Hilo kutokea,alijitazama kwenye mkono wake wa kulia aliona tattoo ya jina la Trevor, Victoria na Trevor walipendana sana mpaka Kila mmoja alichora tattoo ya jina la mwenzie, Victoria alichora tattoo ya jina la Trevor kwenye mkono wake wa kulia karibu na kiganja pia Trevor alichora tattoo ya jina la Victoria upande wa kushoto wa kifua chake,hiyo ilikuwa K**a ahadi ya kupendana na kuwa pamoja siku zote.Victoria alipoitazama tattoo hiyo ghafla alinyanyuka akatoka nje kuelekea msituni hakujali kwamba Ni hatari sana kuelekea msituni muda huo, alitembea mpaka akafika eneo ambalo ajali ya ndege ilitokea miaka 18 iliyopita,alipiga magoti huku machozi yakimtoka Kisha akaanza kufanya maombi kwa ajili ya Trevor sababu uwezekano wa Trevor kuishi ulikuwa Ni mdogo sana

03/04/2019

Sehemu ya 29(the flight to Los Angeles)
Created by ASELI GB (Norman Johnz)
Endelea nayo
Basi Trevor na Victoria walisikia kelele za Isabella waliamka na kukuta Isabella amezimishwa hapohapo Trevor akawauliza "how much do you want (mnataka kiasi gani) huku akiwa anamkinga Victoria ili wasije wakamdhuru lakini wale vijana waliahidiwa kiasi kikubwa Cha pesa na Gabriella endapo tu watamuua Victoria hivyo hawakutaka pesa kwa wakati huo,mmoja wa vijana hao alitoa picha wakaitazama vizuri Kisha wakamtazama Victoria, walipeana ishara kuwa ndiyo yeye,kijana mmoja alimpiga ngumi Trevor lakini Trevor akawa bado anamkinga Victoria,wakamkamata ipasavyo Kisha wakaanza kumpiga ngumi nyingi za tumboni ili aishiwe nguvu,Basi Trevor alikuwa hoi na Victoria alibaki anatetemeka akiwa konani ndipo kijana mmoja akachomoa kisu kwa ajili ya kummaliza Victoria, wakati anataka kumchoma ghafla Trevor alijivuta mbele ya Victoria na kisu kikamchoma yeye badala ya Victoria,wale vijana baada ya kuona kazi imeharibika waliamua kukimbia,kazi iliyobaki Ni kumpeleka Trevor hospitali na je atakufa au atapona.basi Victoria alianza kulia sana huku Trevor damu zilimtoka nyingi mno, punde si punde Isabella alipata fahamu,alivyozinduka akakuta Hali si shwari kabisa aliona Trevor yupo katika Hali mbaya na wasipo kuwa makini atapoteza maisha, Isabella alikuwa na kiasi kidogo Cha pesa, alipiga simu hospitalini ili gari ya kubebea wagonjwa(ambulance)ije kumchukua Trevor aliyekuwa katika Hali mbaya, Trevor alikuwa amezidiwa sana kiasi kwamba muda wake wa kuishi ulikuwa unahesabika.victoria na Isabella walimbeba Trevor kwa shida huku wakilia sana,walifika barabara kuu Kisha wakaanza kulisubiri ambulance,baada ya dakika kumi na Tano ambulance ilifika na kumbeba Trevor, Victoria na Isabella walichukua taxi na kuelekea hospitalini.trevor alivyosikia was hospitalini alifanyiwa matibabu lakini madaktari walionekana kushindwa sababu Trevor alicheleweshwa kufikishwa hospitalini hivyo amepoteza kiasi kikubwa Cha damu,mida ya saa kumi na moja alfajiri Gabriella,Traves na ndugu wengine walifika hospitali baada ya kupewa taarifa kuhusu Trevor baada ya muda kidogo madaktari waliwaeleza kuhusu Hali halisi ya mgonjwa, Gabriella alichanganyikiwa ghafla akamuona Victoria akiwa na Isabella alishangaa sababu alijua Victoria amekwisha uwawa,alianza kuwapiga na kuwatukana ndipo akaja muuguzi wa Trevor,alimueleza kuwa Hawa mabinti ndiyo wamemleta mgonjwa wao hivyo asiwapige Gabriella aliondoka kwa hasira na aibu.

Address

Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Norman johnz posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share