05/03/2025
Kwamba TFF impige mvua ya miaka miwili Kijana wake Ally Kamwe? Nimeona taarifa kwa Ndugu yangu Mkomwa, nimewaza sana kwamba TFF k**a Taasisi yetu tunayoiamini ifikie maamuzi k**a haya? Labda wacha tusubiri taarifa rasmi, lakini k**a ni kweli basi inafikirisha sana.
Kamwe ametiwa hatiani kwa kosa liloitwa la UDHARIRISHAJI, kwamba udharirishaji aliofanya ni kupost โLeo Mjadala redioni 90% ni kuhusu Makolo na Waamuziโ hapo ndipo wakamtia hatiani kwa kudharirisha, lakini nimewaza sana, Ally ni wa kwanza kulaumu? Hao Makolo ni nani? Wanashiriki ligi gani? Ni timu gani? Bado inafikirisha sana, kwamba kuna timu inachezeshwa na Marefa wetu inaitwa Makolo?
Tufanye ni kosa lakini ije na adhabu ya miaka miwili? Nakumbuka kuna Msemaji alifanya kosa k**a hili alifungiwa miezi mitatu, je utofauti wake na Ally ni upi? Miaka miwili imetokana na nini? Je ni TFF tu au kuna Mtu ndani pale au nje yupo nyuma ya mchezo akisukuma kete zake kwa umakini? Ni kosa kubwa kiasi hicho mpaka tumpoteze Kijana wetu kwa miaka miwili?
Kwamba tunashindwa kuvumiliana? Kuadhibiana kwa kuhurumiana? K**a ambavyo Wadau wa soka wamekuwa wakiwavumilia Waamuzi? Sikatai amekosea lakini nakataa ukubwa wa adhabu, sitaki kuamini mpaka nione taarifa rasmi ila k**a kweli ni miaka miwili basi huenda ikawa adhabu kubwa zaidi kuwahi kutolewa kwa kosa dogo zaidi, inafikirisha, siamini k**a taasisi yetu penda ikatoa adhabu k**a hii, unless kuwa na Mtu anashawishi.
Nachofahamu Chura hawezi kuruka mchana wa jua kali tena nchi kavu k**a hakuna kitu kinachomkimbiza.
AMEANDIKA FARHAN JR.