Mtamani Tv

Mtamani Tv MTAMANI TV

24/02/2026

KWELI
Wakati nakua nilifikiri kweli husemwa zaidi na walionizidi umri. Lakini kadili ninavyokua, naendelea kujifunza vitu vingi kuhusu kweli. Yapo ya kushangaza kupita kiasi.

Wakati nakua tulifundishwa kuhusu kuwa wakweli. Tena tulisisitizwa kuwa, kweli inaweza kukupatia furaha ya kudumu.

Cha kushangaza, wakubwa wetu waliotufunza kuhusu kweli wamekengeuka. Na wanatambua kuwa hawasemi kweli lakini tunapokutana nao wanaangusha kilio kana kwamba wanaonyesha upendo juu yetu.

Ina maana kweli tuonyeshe juu Yao na si wao kuonyesha kwetu.

HAYA NI MAAJABU!!!

12/08/2025
MAELEZO YA TAMTHILIA“CHUMBA CHA NJE” SEHEMU YA 05TAMTHILIA YENYE MAUDHUI YA KIMAPENZIAngel anakutana na Mr. 10 na kutaka...
15/07/2025

MAELEZO YA TAMTHILIA
“CHUMBA CHA NJE”
SEHEMU YA 05
TAMTHILIA YENYE MAUDHUI YA KIMAPENZI

Angel anakutana na Mr. 10 na kutaka kukataa kufanya nae mazungumzo. Mr. 10 analazimisha kumsimamisha na kuuliza tatizo.

Six 9 anaingia dukani kwa Mr. Dando na kumpa vitisho Mr. Dando kwa kuwa ni rafiki wa Angel na Angel ana siri zake nyingi.

Baada ya mazungumzo ya Angel na Mr. 10, yanapelekea Mr. 10 kumpa kazi Grey Kiss kuwaweka mbali Angel na Six 9.

Itazame Tamthilia hii inayowavutia wengi mitandaoni iliyotungwa na kuongozwa na Director Mtamani.

MTAMANI TVNDWATI, KIBAHA VIJIJINI – PWANIUsiku wa tarehe 09/07/2025, ulitikiswa na tukio la wizi uliofanywa kwenye duka ...
11/07/2025

MTAMANI TV
NDWATI, KIBAHA VIJIJINI – PWANI

Usiku wa tarehe 09/07/2025, ulitikiswa na tukio la wizi uliofanywa kwenye duka la mwanakijiji cha Ndwati (Jina tunalo) na kupelekea wananchi wenye hasira kali kumdhibiti mmoja wao na alipokuwa mkaidi wakampiga na kupoteza maisha.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti Mtendaji na Mwenyekiti wa Kijiji cha Ndwati, Kibaha Vijijini, Mkoa wa Pwani wamethibitisha kutokea kwa tukio hilo.

Kwa maelezo ya viongozi hao walisema, mwenye Duka anaishi karibu na Duka lake, usiku huo alisikia vishindo vilivyofanya aamke na kwenda Dukani na kukuta watu wawili wanatoka na kufanikiwa kukimbia.

Mmoja alichelewa kutoka na alipotoka alikuta baadhi ya wanakijiji walioshtushwa na mayowe ya mwenye duka kuwa wezi wanaiba kwenye duka lake.

Kitendo hicho kikapelekea kumkimbiza mwizi aliyechelewa kutoka dukani na kufanikiwa kumdhibiti baada ya kumkimbiza k**a urefu wa mita mia moja kutoka dukani.

Baada ya taratibu zote kufanywa na viongozi wa Kijiji cha Ndwati, askari walifika eneo la tukio na Daktari kwa lengo la kuthibitisha k**a kipigo alichopata mwizi kimesababisha afariki au la, na taratibu zingine kufanywa.

Ilipothibitika kuwa mwizi amefariki kutokana na kipigo, na kukutwa na baadhi ya vitambulisho vilivyokuwa na taarifa zake, viongozi wa Kijiji walifanya mawasiliano na kugundua kuwa mwizi alikuwa mwenyeji wa Ngerengere, Mkoa wa Morogoro.

Mawasiliano yalifanyika na ndugu wa marehemu, ndugu walifika eneo la tukio na kukabidhiwa mwili kwa ajili ya mazishi baada ya kupewa taarifa ya tukio.

Hata hivyo, ndugu walielezwa kuwa, endapo watakuwa na jambo lolote linalohusiana na tukio hilo, wafike kituo cha Polisi Kibaha.

MTAMANI TV

MAELEZO YA TAMTHILIA“CHUMBA CHA NJE” SEHEMU YA 04TAMTHILIA YENYE MAUDHUI YA KIMAPENZIPamoja na kufanikiwa kumfikisha Ang...
09/07/2025

MAELEZO YA TAMTHILIA
“CHUMBA CHA NJE”
SEHEMU YA 04
TAMTHILIA YENYE MAUDHUI YA KIMAPENZI

Pamoja na kufanikiwa kumfikisha Angel nyumbani kwake, Six 9 amejikuta anazungumza ukweli unaomsumbua maishani mwake na kumwaga machozi mbele ya Angel.

Grey Kiss anamtembelea Mr. 10 ofisini kwake na kumshauri aachane na Angel.

Mr. 10 anapitiwa usingizi na kujikuta anaota kuwa wanapanga mipango ya kufunga ndoa na Angel. Anastushwa na Angel aliyekuja kuomba ushauri kwa Mr. 10.

Mazungumzo ya Mr. 10 na Angel yanapelekea Angel kutumia nguvu ya k**e ili kuhakikisha Mr. 10 anatoa ushirikiano wa kutosha juu ya tatizo lililofanya afike kwa Mr. 10 kuomba ushauri.

Itazame Tamthilia hii inayowavutia wengi mitandaoni iliyotungwa na kuongozwa na Director Mtamani.

MAELEZO YA TAMTHILIA“CHUMBA CHA NJE” SEHEMU YA 03TAMTHILIA YENYE MAUDHUI YA KIMAPENZISix 9 anakutana na Angel na kumuuli...
07/07/2025

MAELEZO YA TAMTHILIA
“CHUMBA CHA NJE”
SEHEMU YA 03
TAMTHILIA YENYE MAUDHUI YA KIMAPENZI

Six 9 anakutana na Angel na kumuuliza k**a amemdharau au la kuhusu alichomueleza kuwa amtafute jioni ya siku waliokutana.

Wakati Six 9 anamtolea maneno ya vitisho Angel, Mr. Dando anaona tukio hilo lililofanya amtafute Mr. 10 ili amueleze kilichotokea.

Mr. Dando alipokuwa anafikisha ujumbe kwa Mr. 10, anatokea Grey Kiss na kumchukua Mr. 10 ili akaone kinachoendelea kati ya Six 9 na Angel.

Vitisho vinafanya Angel afike nyumbani kwa Six 9

Itazame Tamthilia hii inayowavutia wengi mitandaoni iliyotungwa na kuongozwa na Director Mtamani.

MAELEZO YA TAMTHILIA“CHUMBA CHA NJE” SEHEMU YA 02TAMTHILIA YENYE MAUDHUI YA KIMAPENZIAngel anapata lifti ya Pikipiki ya ...
20/06/2025

MAELEZO YA TAMTHILIA
“CHUMBA CHA NJE”
SEHEMU YA 02
TAMTHILIA YENYE MAUDHUI YA KIMAPENZI

Angel anapata lifti ya Pikipiki ya Grey Kiss akiwa anaelekea kwa Mr. Dando (ambaye ni rafiki yake).

Six 9 anakutana na Angel (Angel) akiwa anaelekea kwa Mr. 10 kujifunza U-Dj. Six 9 anamlazimisha Angel wakutane baadae. Angel anapata hofu kwa namna alivyo Six 9 (Mtu wa mazoezi haswa).

Wakiwa kwenye kilele cha furaha cha mafunzo ya U-Dj, Mr. 10 anamkumbusha Angel juu ya jambo alilowahi kumueleza.

Jibu la Angel kwa Mr. 10, linafanya Mr. 10 ajiulize mara kadhaa na kutaka kumuonyesha Angel uthibitisho.

Itazame Tamthilia hii inayowavutia wengi mitandaoni iliyotungwa na kuongozwa na Director Mtamani.

MTAMANI TVKATA YA PERA, CHALINZE – PWANIMradi unaotekelezwa na Wakandarasi  chini ya Wakala wa Barabara Mijini na Vijiji...
17/06/2025

MTAMANI TV
KATA YA PERA, CHALINZE – PWANI

Mradi unaotekelezwa na Wakandarasi chini ya Wakala wa Barabara Mijini na Vijijini TaRuRa umewafikia wakazi wa Kata ya Pera, Chalinze – Pwani.

Diwani wa Kata ya Pera Mhe. Jackson Mkango, akiongea na Mtamani Tv alieleza kuwa:-

“Mradi unahusisha ufunguzi wa Barabara zenye urefu wa Kilometa 4.3 na uwekaji vifusi katika Kitongoji cha Kilalu.)

Mhe. Mkango anawashukuru wananchi wa Kitongoji cha Kilalu kwa ushirikiano wanaoendelea kutoa ili kufanikisha Mradi kutekelezwa kwa wakati.

Kamati ya ujenzi wa Barabara hizo, pia wanashukuru kwa ushirikiano wanaopata kwa wananchi wa maeneo ya Kitongoji cha Kilalu ambao barabara hizo zinapita karibu na makazi yao.

Baadhi ya wananchi walijitokeza kwenye mradi na kusifu kazi nzuri inayofanywa kwa usimamizi wa Mhe. Jackson Mkango.

Mtamani Tv

Address

Bonyokwa, Ilala
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Mtamani Tv posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Mtamani Tv:

Share