29/05/2025
Serikali imethibitisha kuwa bado kuna mahitaji ya uanzishwaji wa vyuo vya uuguzi na uganga katika maeneo mbalimbali ya nchi, ikiwa ni pamoja na wilaya ya Ukerewe ambapo kwa sasa juhudi zimeelekezwa kwenye ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa katika wilaya hiyo.
Akijibu swali la Mbunge wa Ukerewe, Mhe. Joseph Michael Mkundi, leo Mei 29, 2025 Bungeni Jijini Dodoma, alilyetaka kufahamu ni lini Serikali itajenga tawi la Chuo cha Uuguzi na Uganga Ukerewe, Naibu Waziri wa Afya, Dkt. Godwin Mollel, amesema kuwa Serikali itaendelea kufanya upembuzi yakinifu ili kubaini k**a kuna uhitaji wa kuanzisha Chuo cha Uuguzi katika eneo hilo, mara baada ya kukamilika kwa hospitali hiyo.
“Ni kweli bado kuna mahitaji ya vyuo katika maeneo mbalimbali ya nchi, ila kwa sasa Serikali inajenga hospitali yenye hadhi ya Rufaa ya Mkoa katika wilaya ya Ukerewe. Sambamba na ujenzi huo, Serikali itaendelea kufanya upembuzi yakinifu kuona k**a eneo hilo litahitaji kuwa na Chuo cha Uuguzi,” amesema Dkt. Mollel.