22/04/2018
Kujisifu kuwa umedumu kwenye mahusiano zaidi ya miaka 5 bila kujua hatma na muelekeo wa hayo mahusiona na wala ndugu na wazazi wako hawajui kinachoendelea kwenye maisha yako ya kimahusiano, huo ni UJINGA.
Huwezi ukawa unajisifu upo kwenye mahusiano kwa muda mrefu na mtu asiyetaka muongelee hatma ya hayo mahusiano wala malengo yenu hapo baadae then ukasifu upo katika mikono salama, huko ni kujidanganya.
Si kila uongo hudhihirishwa dhahiri kwa kutamkwa na muongo kuwa huu ni uongo, uongo mwengine unadhihirishwa na vitendo. Huwezi ukaniambia kwamba mnampango wa kutengeneza maisha na mtu asiyetaka kukupeleka kwao kwa miaka yote mliokuwa pamoja kwenye uhusiano, asiyetaka umuulize kuhusu malengo yenu hapo baadae, asiyetaka kuzungumzia hatma na muafaka wa mahusiano yenu, wala asiyetaka kukamilisha ahadi ya lini atakuwa mume wako rasmi.
Miaka inapita umri unasonga, kila umuulizapo utanioa lini utasikia "mwakani", kwa mantiki hiyo huo mwaka mzima utachezewa huku ukingoja MWAKANI ufike ndio ahadi ikamilike, wakati huo jibu k**a hilo ulipewa miaka miwili au mitatu iliyopita.
Kwanini uwendelee kusubiria ahadi zisizofika huku ukiendelea kumjengea uwaminifu kwake kwa kuwakataa watu wenye nia njema na wewe, wanaokufata wakiwa wamejizatiti vyema kuishi na wewe. Kadiri unavyozidi kupotezewa muda wako, kuna akili nyengine huwa inawajia kwenye vichwa vyenu "eti ukiachia mimba ipite itakuwa ni tiketi ya kuolewa haraka". Acha kujidanganya, k**a hana nia ya kukuoa kamwe hawezi kukuoa kwa kumbebea mimba, k**a ulishindwa kushtuka ndani ya miaka mitano iliyopita huku ukiendelea kuchezewa huwezi kumuweza leo ukiwa umeachia mimba ipite.
Ongezeko la singel mathors na watoto wa mitaani linasababishwa na ninyi wasichana kushindwa kufikiria zaidi na kuonesha misimamo yenu angali mapenzi yamekolea. Huu ndio usumbufu mnaompatia leo mkuu wa mkoa Paul Makonda kwa uzembe wenu wa kuforce mwanga kaburini.
Dada zangu wekeni umakini kwenye mahusiano yenu na wapenzi wenu, jaribuni kujitathmini kila wakati, jaribuni kutafakari pamoja na wapenzi wenu hatma ya mahusiano yenu. Acha kujirahisisha kwakuwa umeahidiwa ndoa, ndoa ni mpango wa mungu hauji kwa kubahatisha k**a mchezo wa biko au tatu mzuka, jitengeneze kwanza wewe.
Share
Like Page