12/04/2026
Mwanzo 1:2. Nayo nchi ilikuwa ukiwa, tena utupu, na giza lilikuwa juu ya uso wa vilindi vya maji; Roho ya Mungu ikatulia juu ya uso wa maji.
Tunajifunza uwepo wa mpangilio na mgawanyiko wa vitu katika UUMBAJI, kwanza tuna NCHI, pili MAJI, tatu GIZA.
Katika mpangilio huu Kuna vitu vitatu Mungu alivipanga kwa mfuatano vikiwa vinaelea katika MBINGU (Anga) ambavyo ni NCHI, MAJI na GIZA.
Kwa kuwa Giza lilikuwa juu ya Uso wa vilindi vya maji, Roho ya Mungu (nafsi) ilitulia juu ya uso wa maji ili kuepusha madhara ya giza katika utendaji wake wa kazi kwa kuwa Roho ya Mungu ndio alikuwa ameandaliwa kwa ajiri ya kutoka amri juu ya vitu vyote vitatu ili kuwepo na uwiano mzuri wa kimpangilio na tabia za kimazingira.
NCHI (sayari) zote ziliwekwa katika mfumo wa mfuatano na vitu viwili yaani (Maji na giza), kwahio matukio yanayotokea katika NCHI moja ni sawa kwa NCHI zote isipokuwa tofauti yake ni masaa, siku, mwaka au (muda).
Nuru (Mchana) huifanya Kila NCHI ipate mwanga, joto na tabia za nchi zinazotokana na Nuru asili ambayo ni Jua.
Giza (Usiku) huifanya Kila NCHI ipate Giza ili kupoza joto la Nuru na kufanya tabia ya NCHI husika kutokea au kubalansi kwa usitawi wa viumbe vyake.
Hivyo Kila NCHI hupata Nuru na giza kwa muda tofauti kulingana na mahali au umbali ilipo kutoka chanzo Cha Nuru yaani Jua na mara baada ya Nuru kutoweka Giza huingia mahali Hapo.
Maji husafiri katika Hali mbalimbali kuifikia Kila NCHI, Hali hizo ni kimiminika, yabisi mara chache na mvuke kwa wingi.
Hivyo maji nayo yako katika mzunguko wa kwenda katika NCHI na kurudi katika MBINGU (Anga).
Kwa kukamilisha mifumo hiyo yote ya kutegemeana katika NCHI Roho wa Mungu (nafsi) alibaki juu ya uso wa vilindi vya maji juu yake kukiwa na GIZA anayemruhusu aifikiye Kila NCHI kwa wakati na kuondoka.
Ndipo Roho wa Mungu aliteua baadhi ya NCHI akazipa nafsi kupitia maumbo na matabaka mbalimbali k**a vile binadamu, wanyama, miti na viumbe hai vingine vyote.
Moja ya NCHI iliyopewa nafsi nyingi katika maumbo mbalimbali ni Dunia, NCHI zingine zilipewa nafsi chache na zingine zinautupu zikiwa na nafsi moja kuu peke yake iwezayo kuishi Kila mahali (Roho wa Mungu).
Watu wa Mungu Kila mmoja wetu ni muhimu kujijali na kuyatunza maumbile ya nafsi na NCHI ya mahali alipo ili kuendeleza usitawi wetu wa asili.
Neno NCHI kwa tafsiri ya Roho ya Mungu ni Sayari au umbo lolote lililoko katika MBINGU na lenye uwezo au lisilo na uwezo wa kuizunguka Nuru.
Hivyo NCHI sio hivi vipande vya NCHI moja vinavyogombaniwa na wanadamu hii leo.
NCHI (Sayari) Dunia ni NCHI moja miongoni mwa NCHI nyingi zinazoelea katika MBINGU (Anga).
Inua Huduma kwa Kuisapoti kupitia Akaunti namba 0152418952200 CRDB Benki au Lipa namba ya Vodacom 57241899 Jina Rev.Tr.Pius Kusekwa Elias.
Mawasiliano: +255 785 241 032/+255 755 646 810, Rev.Tr.Pius Kusekwa Elias.
Kanisa la Free Church of Life -FCOL Mji Mwema Laroi Arusha TANZANIA.