01/08/2026
Karibu katika Ibada Maalum ya Kuanza Mwezi wa Nane Itakayofanyika Jumapili hii jioni saa 10:00-12:00 !
Tunakualika kwa moyo wote kuungana nasi katika ibada ya maombi, sifa, kuabudu na Neno la Mungu tunapoanza mwezi wa nane chini ya uongozi wa Roho Mtakatifu.
Katika ibada hii tutamwomba Mungu avunje kila nguvu ya roho ya kukataliwa, aondoe vizuizi vya kiroho, afungue milango ya neema, kibali na mafanikio, na kutuanzishia msimu mpya wa ushindi.
Njoo ukiwa na imani, maana Mungu anaweza kubadilisha historia yako kwa neno moja. Mwezi huu hautakuwa k**a miezi iliyopita—utakuwa mwezi wa kibali, urejesho na ushindi katika jina la Yesu.
Ungana nasi Live Kupitia Youtube , Facebook na Tiktok
Karibu sana! Mungu akubariki.