19/04/2026
“Leo tarehe 20/04 ni siku ya kipekee sana kwangu, siku ambayo Mungu alinijalia zawadi ya uhai. Ninamshukuru kwa neema yake isiyo na kikomo mpaka leo. 🙏
K**a ilivyoandikwa katika Zaburi 118:24 — ‘Hii ndiyo siku aliyoifanya Bwana; tutashangilia na kufurahi ndani yake.’ Leo nachagua kufurahi na kumtukuza Mungu kwa kila hatua ya maisha yangu.
Ninaingia mwaka mpya nikiwa na imani kubwa, nikikumbuka ahadi yake katika Yeremia 29:11 — ‘Maana nayajua mawazo ninayowawazia ninyi… ni mawazo ya amani wala si ya mabaya, kuwapa ninyi tumaini siku zenu za mwisho.’
Naomba baraka zake ziendelee kunifunika, k**a ilivyoandikwa katika Zaburi 23:1 — ‘Bwana ndiye mchungaji wangu, sitapungukiwa na kitu.’
Mwaka huu mpya wa maisha yangu uwe wa mafanikio, afya njema, na ushindi katika kila ninachofanya.
Happy Birthday to me 🎉🔥 Neema juu ya neema, ushindi juu ya ushindi!”