Sogea TV

Sogea TV Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Sogea TV, Photographer, Dar es Salaam.

Kuna tukio la utapeli limetokea Bariadi mkoani Simiyu vijana waliojifanya wataalamu kutoka kampuni za simu wakiwa wameva...
01/05/2026

Kuna tukio la utapeli limetokea Bariadi mkoani Simiyu vijana waliojifanya wataalamu kutoka kampuni za simu wakiwa wamevalia Tisheti zenye majina ya makampuni hayo wamefika kwenye kibanda cha uwakala na kumkuta binti ambaye walimwambia wao ni wataalamu kutoka makampuni hayo na wanatembelea watoa huduma za miamala ili kuwaboreshea laini zao za uwakala

Wakamwambia binti awape namba ya simu ya boss wake waongee nae, wakampigia wakamuuliza tu kwa ufupi wewe ndio fulani mmiliki wa kibanda hiki cha uwakala alivyoongea kuwajibu wakaongea nae k**a salamu za kawaida kwa watoa huduma wakakata simu kisha wakamwambia binti tayari boss wako ameelewa maelekezo tuliyompa atapiga simu akupe maelekezo sasa hivi

Kumbe sauti ya boss wameshaikopi kwenye mfumo wa AI hatimaye wakapigiana kwa sauti ya boss wake na kumpa simu aongee nae binti huyo akawa anaskia sauti ya boss wake kabisa na kupokea maelekezo kwamba "Wape namba za siri hao jamaa na laini za miamala wafanye hayo marekebisho tu nshaongea nao ondoa wasiwasi"

Binti akawapa jamaa wameiba shilingi laki tano 😭😭😭😭😭🙌🙌🙌🙌

NB: Tukio hili limemkuta mtu wangu wa karibu kabisa, sio stori

Mnaofanya biashara ya uwakala chukueni tahadhari, matapeli wamekuja na mbinu mpya wanatumia AI

Rais wa Zanzibar, Dkt. Hussein Mwinyi ametangaza ongezeko la kima cha chini cha mshahara kutoka TZS 300,000 hadi TZS 500...
01/05/2026

Rais wa Zanzibar, Dkt. Hussein Mwinyi ametangaza ongezeko la kima cha chini cha mshahara kutoka TZS 300,000 hadi TZS 500,000 kwa mwezi.

Dkt. Mwinyi amesema kiwango hicho kipya cha mshahara kitaanza kutumika Januari 2027.

_________

Aisee Zanzibar wame Tisha sana

 : Weka maoni yako, Refa ameumudu au hajaumudu mchezo?⏰FT: Yanga SC 0-1 Simba SCSimba wameibuka Mabingwa wa Muungano Cup...
29/04/2026

: Weka maoni yako, Refa ameumudu au hajaumudu mchezo?

⏰FT: Yanga SC 0-1 Simba SC

Simba wameibuka Mabingwa wa Muungano Cup Zanzibar🏆



Benki ya Standard Chartered imeratibu mkopo wa pamoja wa $2.33 bilioni (TZS trilioni 6.07) kwa ajili ya ujenzi wa reli y...
29/04/2026

Benki ya Standard Chartered imeratibu mkopo wa pamoja wa $2.33 bilioni (TZS trilioni 6.07) kwa ajili ya ujenzi wa reli ya kisasa (SGR) nchini Tanzania.

Pazia limefungwa kwa miili yao, lakini nyota zao hazitazimika milele. 🕯️ Hawa ndio Legends wa Bongo Movie walioandika hi...
29/04/2026

Pazia limefungwa kwa miili yao, lakini nyota zao hazitazimika milele. 🕯️ Hawa ndio Legends wa Bongo Movie walioandika historia kwa jasho na damu ili kutupa sisi tabasamu na mafunzo.
Inauma sana kuona picha hii ikiwa na alama ya R.I.P kwa kila mmoja. Hakuna shabiki wa kweli wa filamu anayeweza kusahau mchango wa mashujaa hawa. K**a uliwahi kuguswa na kazi za Steven Kanumba, Mzee Majuto, Mama Grace, au Mzee Hashim Kambi, basi huu ndio wakati wa kuwapa heshima yao ya mwisho.
Usipite bila kusema 'R.I.P' na kuacha 'Like' ya dhati. Mashujaa wetu hawataulika, na historia yao itaishi vizazi na vizazi! 🕊️💔🙏"

28/04/2026
HALMASHAURI ya Wilaya ya Ludewa mkoani Njombe imelalamikia ongezeko la watumishi wanaoomba uhamisho muda mfupi baada ya ...
28/04/2026

HALMASHAURI ya Wilaya ya Ludewa mkoani Njombe imelalamikia ongezeko la watumishi wanaoomba uhamisho muda mfupi baada ya kuajiriwa, hali inayodaiwa kudhoofisha utoaji wa huduma.

Kwa mujibu wa halmashauri hiyo, katika kipindi cha mwaka wa fedha kuanzia Julai 2025 hadi Machi 2026, jumla ya watumishi 61 wamehama kutoka wilayani humo, huku waliohamia wakiwa sita pekee.

Akizungumza mwishoni mwa wiki katika kikao cha Baraza la Madiwani diwani wa kata ya Luana, Wilbard Mwinuka alisema hali hiyo imekuwa kikwazo kikubwa kwa maendeleo ya wilaya.

“Kulikuwa na utaratibu wa mtu anayehama kutafuta mbadala wa kuja kuchukua nafasi yake, lakini sasa haupo. Watu wanaondoka bila kuzibwa pengo, huku wengine wakistaafu, kuugua au kufariki. Hili linakuwa kero kubwa,” alisema Mwinuka.

Aliongeza kuwa tatizo hilo linaathiri zaidi maeneo ya vijijini ambako upungufu wa watumishi ni mkubwa.

“Huku vijijini kuna shule zina walimu wawili tu, mmoja analazimika kufundisha darasa la kwanza hadi la saba. Tunaomba wabunge watusaidie, maana sisi ni wahanga wakubwa,” alieleza.

Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo, Edger Mtitu, alisema suala hilo lilijadiliwa kwa kina katika k**ati mbalimbali kutokana na athari zake.

“Inaonyesha wazi kuwa watumishi wanaoajiriwa Ludewa hawakai. Tunashukuru kwa ajira mpya 122, lakini tayari 61 wameondoka. Hii inarudisha nyuma jitihada zetu,” alisema.

Naye Mbunge wa Ludewa, Joseph Kamonga, alisema utafiti unaonyesha sababu kubwa ya watumishi kuhama ni tatizo la miundombinu.

“Tatizo la barabara, umeme na maji katika baadhi ya maeneo linachangia watumishi kushindwa kudumu. Ni lazima tuboreshe miundombinu hii ili kuwavutia na kuwabakiza,” alisema Kamonga.

Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo, Wise Mgina, aliwataka wabunge kushirikiana kuishughulikia adha hiyo, akisema hali inaendelea kuwa mbaya.

Address

Dar Es Salaam

Telephone

+255684704255

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Sogea TV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Sogea TV:

Share

Category