18/09/2025
Ity tunafanya kazi pia ya kutekeleza haki za watoto .
Haya ni baadhi ya makundi ya Tasisi yetu yaliyoweza kutoa tabasamu kwa watoto mbalimbali waliweza kula na kunywa na watoto na kuwapa mahitaji mbalimbali ya muhimu
Kupitia hili naomba nikumbushe :-
FAHAMU SHERIA ZA MSINGI ZA MTOTO
1. Mtoto ana haki ya kupewa jina na utaifa
Sheria ya Mtoto ya Sura ya 20 ya Mwaka 2009, kifungu cha 6 mtoto ana haki ya kuwa na utaifa, kupewa jina na kuwafahamu wazazi wake wa kibaiolojia.
2. kila mtoto ana haki ya kutoa maoni yao
Sheria ya Mtoto Sura ya 20 ya mwaka 2009, kifungu cha 11, mtoto ana haki ya kutoa maoni na maoni yake yapaswa kusikilizwa, kuheshimiwa na pia kupewa nafasi ya kushiriki kwenye kufanya maamuzi yatakayo pelekea ustawi wake.
3. Matunzo ya mtoto
Sheria ya Mtoto Sura ya 20 ya mwaka 2009, kifungu cha 17 inamtaka mtu yeyote anayemiliki sehemu ya starehe ikiwemo bar, au kilabu kutowaruhusu watoto kuingia maeneo hayo.
o Vile vile asiwauzie watoto sigara, pombe au kilevi cha aina yoyote. Na mtu atakaye kwenda kinyume na kifungu hicho tajwa atakuwa amefanya makosa na adhabu yake haitakuwa chini ya shilingi Milioni moja na isiyozidi milioni tano au kifungo jela kwa kipindi kisichopungua miezi kumi na mbili.
4. Amri ya malezi ya Mahak**a iwe kwa faida ya mtoto
Sheria ya Mtoto Sura ya 20 ya mwaka 2009, kifungu cha 18 Mahak**a inaweza kuamua mtoto akae sehemu nyingine tofauti na wazazi wake k**a wazazi wake wapo hai ikiwa mahak**a itathibitisha kuwa usalama wa mtoto upo hatarini.
5. Amri ya matunzo na uasili wa mtoto
Sheria ya Mtoto Sura ya 20 ya mwaka 2009, kifungu cha 24, yakuwa ikiwa wazazi, walezi au ndugu wa mtoto ambaye yupo chini ya amri ya uangalizi hawaonyeshi kuwa na hali ya kujali maslai ya mtoto kwa namna yoyoyte kwa kipindi cha uangalizi kilichotolewa na mahak**a, mtoto anaweza kuasiliwa (adoption) na mlezi mweingine.
6. Haki ya mtoto pindi wazazi wanapotengana
Sheria ya ndoa ya Tanzania wazazi wakitengana kwa talaka mtoto ana haki ya;
-Kuendelea kupata elimu ya kiwango kilekile alichokuwa akikipata kabla ndoa ya wazazi wake haijavunjika.
-Kuishi na mzazi ambaye kwa maoni ya mahak**a ana uwezo wa kumtunza mtoto na uwezo wa kuzingatia maslahi bora ya motto.
-Na awe na uwezo wa kumtembelea mzazi mwingine wakati wowote atakapojisikia kufanya hivyo, ikiwa tu kufanya hivyo kutaingiliana na ratiba za shule au masomo.