03/06/2026
Kulikuwa na kijana mmoja katika mtaa wa Kibera aliitwa Ezekiel. Ezekiel alikuwa kijana wa kawaida, lakini alikuwa na tabia ya ajabu ambayo watu wengi hawakuielewa. Alipenda kula panya kwa siri.
Kila usiku, Ezekiel angeonekana akizunguka karibu na vibanda vya sokoni akiwa na mfuko wake mweusi. Watu walidhani anatafuta chuma chakavu, lakini ukweli ni kwamba alikuwa akiwinda panya wakubwa wa mitaani.
Siku moja rafiki yake wa karibu, Kevin, alimfuata kwa siri.
“Bro, unaenda wapi usiku kila siku?” Kevin aliuliza.
Ezekiel akajibu kwa sauti ya chini, “Usipige kelele… leo nitakushow siri yangu.”
Walifika nyuma ya kibanda cha chips. Ezekiel akatoa panya mkubwa ndani ya mfuko.
Kevin akaruka kwa hofu. “Wewe ni mchawi ama nini?”
Ezekiel akaanza kucheka. “Hapana bana! Nilianza kula panya wakati nilikuwa mdogo ushago. Babu alisema nyama yake huongeza nguvu.”
Kevin hakuamini. Lakini siku hiyo Ezekiel alipika panya kwa viungo nyingi mpaka harufu ikaanza kusambaa mtaa mzima.
Majirani wakaanza kuuliza: “Nani anapika nyama tamu hivi?”
Kevin akasema kwa siri: “Msijue tu ni nyama gani…”
Baada ya kula, Kevin alikiri kwa aibu: “Eeh… si mbaya vile nilifikiria.”
Habari zikasambaa mtaani haraka. Watu wakaanza kumuita “Ezekiel Ratatouille.”
Lakini siku moja mambo yaliharibika. Panya mmoja aliyemshika alikuwa ametoka kwa duka la sumu. Ezekiel alianza kuumwa tumbo vibaya na kukimbizwa hospitali.
Daktari alimwangalia na kusema: “Wewe ulikula nini?”
Ezekiel akanyamaza.
Kevin akasema: “Doctor… ni panya.”
Daktari akatoa miwani polepole na kusema: “Kuanzia leo, ukitaka protein kula maharagwe!”
Baada ya tukio hilo, Ezekiel aliacha kula panya na akaanza biashara ya kuuza smokie na mayai. Lakini mpaka leo, watu wa mtaa bado humcheka wakisema:
“Ficha chakula, Ezekiel anakuja!” ZACK TV